Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

ENDELEA KUKESHA!

Mashambulizi Shuleni—Biblia Inasema Nini?

Mashambulizi Shuleni—Biblia Inasema Nini?

 Mei 24, 2022, tukio lenye kusikitisha sana lilitokea huko Uvalde, Texas, Marekani. Gazeti la The New York Times liliripoti hivi: “Mwanamume mmoja aliwaua kwa bunduki watoto 19 na walimu wawili. . . katika shule ya Msingi ya Robb.”

 Inasikitisha kwamba mambo kama hayo yenye kuogopesha hutukia mara nyingi. Gazeti la USA Today linaeleza kwamba katika Marekani tu, mwaka jana kulikuwa na visa 249 vya mashambulizi ya bunduki vilivyotokea shuleni, vilikuwa vingi zaidi kuliko mwaka mwingine wowote tangu 1970.

 Kwa nini mambo hayo yenye kusikitisha yanatokea? Tunaweza kukabilianaje na matukio hayo yenye kuhuzunisha? Je, kuna tumaini lolote kwamba ukatili utakwisha? Biblia inatupatia majibu.

Kwa nini ukatili unazidi kuongezeka ulimwenguni?

  •    Biblia inakiita kipindi tunachoishi kuwa “siku za mwisho” wakati ambapo watu wengi wangekuwa “wakali” na “wasio na upendo wa asili,” na wangefanya matendo mengi ya kikatili. Watu hao wangeendelea “kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi.” (2 Timotheo 3:1-5, 13) Ili kujifunza mengi zaidi, soma makala yenye kichwa, “Je, Biblia Ilitabiri Mitazamo na Matendo ya Watu Leo?

 Watu wengi hujiuliza, ‘Kwa nini Mungu hazuii matukio yenye kusikitisha kama vile mashambulizi shuleni, yasitokee? Ili kupata jibu kutoka kwa Biblia, soma makala yenye kichwa, “Kwa Nini Watu Wazuri Hupatwa na Mambo Mabaya?

Tunaweza kukabilianaje na matukio hayo yenye kuhuzunisha?

  •    “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha, ili . . . kupitia faraja kutoka kwa Maandiko tuwe na tumaini.”​—Waroma 15:4.

 Kanuni za Biblia zinaweza kukusaidia kukabiliana na ukatili unaoendelea ulimwenguni. Ili kupata habari zaidi soma gazeti la Amkeni! lenye kichwa, “Je, Jeuri Itawahi Kwisha?

 Ili kupata mapendekezo ya jinsi wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao kukabiliana na ripoti zenye kuogopesha katika taarifa za habari, soma makala yenye kichwa “Je, Taarifa za Habari Zenye Kuogopesha Zinawaathiri Watoto Wako?

Je, ukatili utakwisha?

  •    “Atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”​—Zaburi 72:14.

  •    “Watafua panga zao ziwe majembe ya plau na mikuki yao iwe miundu. Taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”​—Mika 4:3.

 Mungu atatimiza mambo ambayo wanadamu hawana uwezo wa kufanya. Ufalme wake ambao ni serikali kutoka mbinguni utaangamiza silaha zote na kukomesha ukatili. Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza, soma makala yenye kichwa, “Wakati Huo ‘Amani Itakuwa Nyingi.’