Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Francesco Carta fotografo/Moment via Getty Images

Tatizo Linalozidi Kuongezeka la Upweke—Biblia Inasema Nini

Tatizo Linalozidi Kuongezeka la Upweke—Biblia Inasema Nini

 Kulingana na ripoti ya karibuni ya ulimwenguni pote, a karibu mtu mmoja kati ya wanne anajihisi mpweke.

  •    “Kujitenga kijamii kunaweza kumwathiri mtu yeyote, wa umri wowote, popote alipo.”​—Chido Mpemba, mwenyekiti msaidizi wa Tume ya Mahusiano ya Kijamii ya Shirika la Afya Ulimwenguni.

 Watu wengi hufikiri kwamba upweke huwaathiri wazee au watu walio peke yao. Lakini hata vijana, watu wenye afya nzuri, waliofanikiwa, na waliofunga ndoa wanaathiriwa na upweke. Kujitenga kijamii na upweke kunaweza kuathiri vibaya afya ya mtu ya kimwili na ya kihisia.

  •    Dakt. Vivek Murthy, daktari mkuu wa upasuaji nchini Marekani anasema hivi: “Upweke unahusisha mengi zaidi kuliko kuwa na hisia mbaya tu.” Anaongezea hivi: “Hatari ya kufa kutokana na kujitenga kijamii inalingana na ile inayosababishwa na kuvuta sigara 15 kila siku.”

Biblia inasema nini?

 Muumba wetu hataki tujitenge kijamii. Kusudi la Mungu sikuzote limekuwa kwamba wanadamu wafurahie ushirika mzuri na wenye kuridhisha.

  •    Kanuni ya Biblia: “Mungu akasema: ‘Si vema mwanamume huyu aendelee kuwa peke yake.’”​—Mwanzo 2:18.

 Mungu anataka tusitawishe uhusiano pamoja naye. Anaahidi kutukaribia iwapo tutafanya jitihada ya kumkaribia yeye.​—Yakobo 4:8.

  •    Kanuni ya Biblia: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao.”​—Mathayo 5:3.

 Mungu anataka tumwabudu pamoja na wengine. Tunapofanya hivyo, tunajihisi vizuri zaidi kihisia.

  •    Kanuni ya Biblia: “Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukutana pamoja, . . . bali tutiane moyo.”​—Waebrania 10:24, 25.

 Ili upate habari zaidi kuhusu kwa nini ni muhimu kupambana na upweke, soma makala yenye kichwa “Upweke Katika Ulimwengu Uliojaa Mawasiliano.”