Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kim Steele/The Image Bank via Getty Images

KAMPENI YA PEKEE

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini Kuhusu Matatizo ya Kiuchumi?

Ufalme wa Mungu Utafanya Nini Kuhusu Matatizo ya Kiuchumi?

 Watu wengi ulimwenguni wanapambana kupata pesa za kutosha kukidhi mahitaji yao, na hali zinazidi kuwa ngumu.

  •   Kulingana na ripoti moja ya karibuni, a ulimwenguni pote “thamani ya pesa ambazo watu wanapata kila mwezi imepungua.” Ripoti hiyo inaonya kwamba ikiwa hakuna jambo litakalofanywa, kutakuwa na tofauti kubwa zaidi kati ya matajiri na maskini, na “kiwango cha maisha cha wafanyakazi wengi na familia zao” kitashuka.

 Je, serikali zitaweza kutatua tatizo hilo la kiuchumi linalozidi kuongezeka au hata kulipunguza?

 Biblia inaeleza kwamba kuna serikali ambayo inaweza kutatua matatizo yote ya kiuchumi kutia ndani ukosefu wa usawa, na itafanya hivyo. Inasema kwamba “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme,” serikali moja ambayo itashughulikia mambo yote duniani. (Danieli 2:44) Serikali hiyo itakapoutawala ulimwengu wote, hakuna mtu atakayesahauliwa au kuachwa nyuma. (Zaburi 9:18) Ufalme wa Mungu utahakikisha kwamba raia wake wanapata kila kitu wanachohitaji ili wawe na furaha. Watu wote watafurahia matokeo ya kazi yao ngumu.—Isaya 65:21, 22.

a Ripoti ya 2022-2023 ya Shirika la Kimataifa la Wafanyakazi Kuhusu Mishahara ya Ulimwenguni Pote