Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

YURI LASHOV/AFP via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Wakristo na Vita—Biblia Inasema Nini?

Wakristo na Vita—Biblia Inasema Nini?

 Kama ambavyo tumeona wakati wa vita nchini Ukrainia, viongozi wengi Wakristo wanawatia watu moyo waunge mkono upande fulani katika vita hivyo. Ona jinsi viongozi wa dini wameunga mkono pande zote:

  •   “Ni heshima na shukrani kubwa kwa mashujaa wote wanaotetea nchi yao ya Ukrainia kutokana na mkandamizaji . . . Sikuzote mioyo yetu, sala zetu, na utegemezo wetu upo pamoja nanyi.”​—Askofu Epiphanius wa Kwanza wa Kyiv, kama ilivyoripotiwa katika The Jerusalem Post, la Machi 16, 2022.

  •   “Mkuu wa Kanisa Othodoksi la Urusi aliongoza ibada ya pekee kwa ajili ya wanajeshi wa Urusi Jumapili na kuwatia moyo wailinde nchi yao ‘kama Warusi tu wanavyoweza’ huku Moscow ikiendeleza kampeni yake nchini Ukrainia.​—Shirika la Habari la Reuters, Aprili 3, 2022.

 Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika vita? Biblia inasema nini?

Kile ambacho Biblia inasema hasa

 Biblia inaonyesha kwamba wale ambao ni wafuasi wa kweli wa Yesu Kristo hawajihusishi katika vita.

  •   “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wote wanaochukua upanga wataangamia kwa upanga.”​—Mathayo 26:52.

     Je, kweli mtu anayeunga mkono vita au anayepigana katika vita anatii maneno ya Yesu?

  •   “Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda, nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu—mkiwa na upendo miongoni mwenu.”​—Yohana 13:34, 35.

     Je, mtu anayeunga mkono upande fulani katika vita anaonyesha upendo ambao Yesu alisema ungewatambulisha wanafunzi, au wafuasi wake?

 Ili upate habari zaidi, soma makala yenye kichwa “Je, Ukristo Unaunga Mkono Vita?

Wakristo na vita leo

 Je, inapatana na akili kuwatazamia Wakristo kutojihusisha katika vita leo? Ndiyo. Biblia ilitabiri kwamba katika siku zetu, kipindi kinachoitwa “siku za mwisho,” kungekuwa na watu kutoka katika mataifa yote ambao kupatana na mafundisho ya Yesu, “hawatajifunza vita tena kamwe.”​—Isaya 2:2, 4.

 Hivi karibuni Yehova, a yule “Mungu wa amani,” atatumia serikali yake ya mbinguni kuwakomboa watu “kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”​—Wafilipi 4:9; Zaburi 72:14.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.