Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Pawel Gluza/500Px Plus/Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Wanyamapori Wamepungua kwa Asilimia 73 Ndani ya Miaka 50—⁠Biblia Inasema Nini?

Wanyamapori Wamepungua kwa Asilimia 73 Ndani ya Miaka 50—⁠Biblia Inasema Nini?

 Oktoba 9, 2024, Shirika la Hazina ya Wanyamapori Ulimwenguni lilitoa ripoti yenye kusikitisha kuhusu athari za shughuli za wanadamu kwa wanyamapori. Ripoti hiyo ilisema kwamba “katika miaka 50 iliyopita (1970-2020), kwa wastani idadi ya wanyamapori imepungua kwa asilimia 73.” Ripoti hiyo ilionya hivi: “Hakuna shaka kwamba mambo tutakayofanya ndani ya miaka mitano ijayo yataathiri sana jinsi maisha yatakavyokuwa hapa Duniani.”

 Watu wengi wanaposikia ripoti kama hizo wanashtuka. Hilo linaeleweka kwa sababu tunaipenda sayari yetu maridadi na hatutaki kuona wanyamapori wakiumia. Tunahisi hivyo kwa sababu Mungu alituumba tukiwa na tamaa ya kuwatunza wanyama.—Mwanzo 1:27, 28; Methali 12:10.

 Hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Je, tutaweza kuwalinda wanyama walio duniani? Biblia inasema nini?’

Tumaini la wakati ujao

 Licha ya jitihada zetu za kuwaokoa wanyama, ukweli ni kwamba ni Mungu tu anayeweza kuwalinda wanyamapori kikamili. Katika Ufunuo 11:18, Biblia ilitabiri kwamba Mungu ‘atawaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ Mstari huo unatufundisha mambo mawili:

  1.  1. Mungu atawazuia wanadamu wasiiharibu dunia kabisa au kuiangamiza.

  2.  2. Mungu atachukua hatua hivi karibuni. Tunajuaje hilo? Tuna uhakika kwa sababu leo kuna hatari kubwa zaidi ya wanadamu kuwaangamiza wanyamapori kuliko wakati mwingine wowote.

 Mungu atafanya nini ili kuleta suluhisho? Ataitawala dunia nzima kupitia serikali, au Ufalme wake wa mbinguni. (Mathayo 6:10) Serikali hiyo itawafundisha wanadamu watiifu jinsi ya kuwatunza na kuwalinda wanyama duniani.—Isaya 11:9.