Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

hadynyah/E+ via Getty Images

ENDELEA KUKESHA!

Ukosefu wa Chakula Ulimwenguni Unatokezwa na Vita na Mabadiliko ya Hali ya Hewa—Biblia Inasema Nini?

Ukosefu wa Chakula Ulimwenguni Unatokezwa na Vita na Mabadiliko ya Hali ya Hewa—Biblia Inasema Nini?

 Vita nchini Ukrainia, pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa, yanaendelea kusababisha upungufu mkubwa wa chakula ulimwenguni. Hilo ni kweli hasa katika nchi zinazoendelea ambako ni vigumu kwa watu wengi kupata chakula cha kutosha.

  •   “Utokezwaji na upatikanaji wa chakula unaathiriwa sana na vita, mabadiliko ya hali ya hewa, kupanda kwa gharama za mafuta na mambo mengine.”​—António Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Julai 17, 2023.

  •   “Wataalamu wanatabiri kwamba kujiondoa kwa Urusi katika mkataba wa kusambaza nafaka kutaathiri vibaya tatizo la upungufu wa chakula ulimwenguni na kufanya gharama za chakula zipande katika nchi zilizo na hali ngumu ya kiuchumi, hasa Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati.”​—Atalayar.com, Julai 23, 2023.

 Fikiria kile ambacho Biblia inasema kuhusu tatizo la chakula na wakati ujao.

Biblia ilitabiri kuhusu tatizo la chakula

  •   Yesu alitabiri hivi: “Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula.”​—Mathayo 24:7.

  •   Kitabu cha Biblia cha Ufunuo kinazungumza kuhusu wapanda-farasi wanne wa mfano. Mmoja kati ya wapanda-farasi hao anawakilisha vita. Anafuatwa na mwingine anayefananisha njaa, wakati ambapo chakula kitapimwa na kuuzwa kwa bei ya juu kupita kiasi. “Nikaona, . . . farasi mweusi, na yule aliyeketi juu yake alikuwa na mizani mkononi mwake. Nami nikasikia kitu kama sauti . . . ikisema: ‘Kibaba cha ngano kwa dinari moja [au, mshahara wa siku moja] na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja.’​—Ufunuo 6:5, 6.

 Unabii huo wa Biblia kuhusu ukosefu wa chakula unatimizwa sasa katika wakati ambao Biblia inauita “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1) Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu “siku za mwisho” na hao wapanda-farasi wanaotajwa katika Ufunuo, tazama video Ulimwengu Umebadilika Tangu Mwaka wa 1914 na usome makala yenye kichwa “Wapanda Farasi Wanne​—Jinsi Wanavyokuhusu.”

Jinsi Biblia inavyoweza kukusaidia

  •   Biblia ina mashauri yanayofaa yanayoweza kutusaidia kukabiliana na hali ngumu, kutia ndani kupanda kwa bei za chakula au hata upungufu wa chakula. Ona mifano kadhaa katika makala yenye kichwa “Jinsi ya Kuishi Ukiwa na Pesa Kidogo.”

  •   Pia Biblia inatupatia tumaini kwamba mambo yatakuwa mazuri zaidi. Inaahidi wakati ambapo “kutakuwa na nafaka nyingi duniani” na kila mtu atakuwa na chakula kingi. (Zaburi 72:16) Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu tumaini hilo la wakati ujao na kwa nini unaweza kuwa na uhakika litatimia, soma makala yenye kichwa “Tumaini Bora la Wakati Ujao.”