Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 146

Vitu Vyote Kuwa Vipya

Vitu Vyote Kuwa Vipya

(Ufunuo 21:1-5)

  1. 1. “Ishara za nyakati” zaonyesha:

    Ufalme wa Mungu watawala.

    Mbinguni vita vimepiganwa.

    Mapenzi ya Mungu yatafanywa

    (KORASI)

    Shangilieni kwa kuwa,

    Mungu akaa na watu.

    Maumivu hayatakuwapo,

    Wala machozi, kifo, kilio;

    Mungu asema: ‘Nafanya vipya.

    Yote hayo ni kweli.’

  2. 2. Tazameni Yerusalemu Jipya,

    Bi-harusi wa Mwana-Kondoo.

    Amepambwa mawe ya thamani,

    Na mwangaza wake ni Yehova.

    (KORASI)

    Shangilieni kwa kuwa,

    Mungu akaa na watu.

    Maumivu hayatakuwapo,

    Wala machozi, kifo, kilio;

    Mungu asema: ‘Nafanya vipya.

    Yote hayo ni kweli.’

  3. 3. Jiji hilo kuwapendeza wote.

    Malango kuwa wazi daima.

    Mataifa kuenda nuruni.

    Watumishi wa Mungu mwangaze.

    (KORASI)

    Shangilieni kwa kuwa,

    Mungu akaa na watu.

    Maumivu hayatakuwapo,

    Wala machozi, kifo, kilio;

    Mungu asema: ‘Nafanya vipya.

    Yote hayo ni kweli.’