Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 17

‘Nataka’

‘Nataka’

(Luka 5:13)

  1. 1. Upendo wa Kristo Yesu,

    Ulimchochea kuja.

    Katujali sana,

    toka moyoni,

    Kwa maneno na matendo.

    Wagonjwa aliwaponya,

    Viziwi, vipofu pia.

    Kazi yake aliitimiza.

    Na alisema: ‘Nataka.’

  2. 2. Tumwige Mwana wa Mungu,

    Kila siku maishani.

    Tuonyeshe watu

    tunawapenda,

    Neno Lake wajifunze.

    Fadhili tuwaonyeshe,

    Kwa maneno na matendo.

    Wajane nao yatima pia,

    Tuwaambie: ‘Nataka.’