WIMBO NA. 90
Tianeni Moyo
-
1. Tuwatiapo ndugu moyo,
Kumtumikia Mungu,
Upendo unaimarika;
Kwawa amani, umoja.
Upendo wa watu wa Mungu,
Hufanya tuvumilie.
Kutaniko ni kimbilio,
Mahali pa usalama.
-
2. Neno zuri linaposemwa,
Lafurahisha moyo, we!
Maneno yenye kufariji
Ya ndugu zetu wapendwa.
Tufanyapo kazi pamoja,
Na ndugu na dada zetu,
Tunaimarishana nao,
Mizigo twabebeana.
-
3. Siku ya Yehova karibu.
Twaiona kwa imani.
Tunahitaji mikutano,
Tubaki katika njia.
Milele tutatumikia,
Na watu wake Yehova.
Daima tutiane moyo,
Tuwe washikamanifu.
(Ona pia Luka 22:32; Mdo. 14:21, 22; Gal. 6:2; 1 The. 5:14.)