Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha​—Video

Sitawisha ustadi muhimu wa kusoma na kufundisha mbele ya watu.

SOMO LA 1

Utangulizi Wenye Matokeo

Unawezaje kuwafanya wasikilizaji wako watamani kusikia unachotaka kusema?

STUDY 2

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Unaweza kufanya nini ili wasikilizaji wako wastarehe unapozungumza nao?

SOMO LA 3

Kutumia Maswali

Unawezaje kutumia maswali kujadiliana na wasikilizaji wako, kudumisha upendezi wao, na kukazia mambo muhimu?

SOMO LA 4

Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko

Unaweza kufanya nini ili kutayarisha akili za wasikilizaji wako ili wafaidike kikamili na mistari ya Biblia unayosoma?

STUDY 5

Kusoma kwa Usahihi

Ni mbinu zipi zinazoweza kutusaidia kusoma kwa sauti kile hasa ambacho kimeandikwa kwenye ukurasa?

SOMO LA  6

Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Unapaswa kufanya nini unaposoma andiko mbele ya wasikilizaji na pia baada ya kusoma andiko hilo, utafanya nini ili uwasaidie kuelewa sababu ya kulisoma?

SOMO LA 7

Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Unaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba hupotoshi kweli?

SOMO LA 8

Mifano Inayofundisha

Unaweza kufanya nini ili kutumia mifano kwa njia nzuri kama yule Mwalimu Mkuu?

SOMO LA 9

Kutumia Picha na Video Vizuri

Unaweza kutumiaje picha na video kuwasaidia wasikilizaji wako waelewe mambo makuu?

SOMO LA 10

Ubadilifu wa Sauti

Unawezaje kutumia ubadilifu wa sauti kuwasilisha mawazo waziwazi na kuchochea hisia za wasikilizaji wako?

SOMO LA 11

Shauku

Unawezaje kutumia shauku kuwachangamsha na kuwachochea wasikilizaji wako?

SOMO LA 12

Kuzungumza kwa Hisia

Unawezaje kuwaonyesha wasikilizaji wako hisia zinazotoka moyoni?

SOMO LA 13

Kuonyesha Wasikilizaji Manufaa ya Habari Unayozungumzia

Unawezaje kuzungumzia habari kwa njia ambayo itawasaidia wasikilizaji wako waelewe manufaa yake na wachochewe kuchukua hatua?

SOMO LA 14

Kukazia Mambo Makuu

Wasaidie wasikilizaji wako wakazie uangalifu, waelewe, na kukumbuka mambo unayosema kwa kukazia mambo makuu.

SOMO LA 15

Kuzungumza kwa Usadikisho

Unaweza kuzungumzaje kwa usadikisho unapotoa hotuba au unapokuwa utumishini?

SOMO LA 16

Uwe Mwenye Kujenga na Mwenye Kutia Moyo

Ni mambo gani matatu ambayo yatatusaidia kuzungumza kwa njia ambayo itaboresha hali na kuchochea wasikilizaji?

SOMO LA 17

Habari Inayoeleweka

Ni mambo gani unayopaswa kuepuka unapojaribu kuwasaidia wasikilizaji wako waelewe maana ya ujumbe wako?

SOMO LA 18

Kuwaelimisha Wasikilizaji

Unaweza kufanya nini ili uwachochee wasikilizaji wako kufikiri na kuwafundisha jambo muhimu?

SOMO LA 19

Kujitahidi Kugusa Moyo

Unawezaje kuwachochea wasikilizaji wako wawe na nia nzuri?

SOMO LA 20

Umalizio Wenye Matokeo

Unapaswa kutimiza nini katika umalizio wako iwe uko kutanikoni au katika huduma?

Huenda Ukapenda Pia

VITABU NA BROSHUA

Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha

Chapisho hili limekusudiwa kukusaidia uboreshe ustadi wako wa kusoma mbele ya watu na kuboresha ufundi wako wa kusema na kufundisha.