Andiko la Mwaka wa 2015
“Mshukuruni Yehova, kwa maana yeye ni mwema.” Zaburi 106:1
Baada ya kukombolewa kutoka mikononi mwa Farao na jeshi lake katika Bahari Nyekundu, Waisraeli walikuwa na kila sababu ya kumshukuru Yehova. Sisi pia tunaweza kumshukuru Yehova. Ni kweli kwamba tunaweza kuvunjika moyo tunapokabili hali ngumu maishani. Nyakati kama hizo, tunafarijiwa na kuimarishwa kwa kutafakari kuhusu baraka tulizo nazo.
Zab. 46:1) Kukazia macho baraka hizo kutatusaidia tufanikiwe hata tunapokabili hali ngumu sana. Katika mwaka wa 2015, na tutafakari kwa shangwe baraka tulizo nazo na tuchochewe ‘kumshukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema; kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.’—Zab. 106:1.
Mojawapo ya baraka bora tulizo nazo ni tumaini letu hakika la kuondolewa kwa mambo yote yanayotusababishia maumivu na taabu. Hata tukabili hali ngumu kadiri gani, tunajua kwamba Yehova hatatuacha. Mchungaji wetu mwenye upendo hutupatia kila kitu tunachohitaji ili tumtumikie kwa uaminifu. Sikuzote amekuwa “kimbilio na nguvu, msaada unaopatikana kwa utayari wakati wa taabu.” (