Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MATUKIO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA

Mkutano Mkubwa Zaidi wa Mashahidi wa Yehova

Mkutano Mkubwa Zaidi wa Mashahidi wa Yehova

JUMAMOSI, Oktoba 5, 2013, watu 257,294 kutoka nchi 21 walihudhuria mkutano wa 129 wa kila mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Baadhi ya wasikilizaji hao walikuwepo kwenye mkutano huo na wengine walisikiliza moja kwa moja kupitia Intaneti. Mwisho juma uliofuata, Mashahidi wengine waliokusanyika walitazama rekodi ya programu hiyo. Kwa ujumla, watu 1,413,676 kutoka nchi 31 walisikiliza programu hiyo—hakujawahi kuwa na mkutano mkubwa hivyo wa Mashahidi wa Yehova.

Tangu miaka ya 1920, Mashahidi wa Yehova wametangaza programu za makusanyiko kupitia simu na vituo vya redio kwa wasikilizaji walio maeneo mbalimbali duniani. Sasa, teknolojia ya Intaneti imefanya iwe rahisi hata kwa watu wanaoishi mbali sana kusikiliza na kuona matukio yanapofanyika au baadaye kidogo.

Washiriki wa ofisi kadhaa za tawi walifanya kazi kwa zaidi ya mwaka ili kuunda mfumo wa kupeperusha video kupitia Intaneti. Katika mwisho juma wa mkutano huo wa mwaka, mafundi wa mitambo walielekeza mfumo wa kupeperusha programu hiyo wakiwa jijini Brooklyn, New York, na walifanya kazi usiku na mchana kwa kuwa programu hiyo ilionyeshwa katika maeneo 15 mbalimbali duniani yanayotofautiana kwa saa.