INDONESIA
Yehova Ametubariki Zaidi ya Tulivyotarajia!
Angeragō Hia
-
ALIZALIWA 1957
-
ALIBATIZWA 1997
-
HISTORIA FUPI Alirudi kijijini kwao Kisiwani Nias na kuanzisha kutaniko.
MWAKA wa 2013, kutaniko letu dogo la Tugala Oyo lilipokea habari yenye kusisimua za kujengewa Jumba jipya la Ufalme! Viongozi wa eneo hilo walikubali mradi huo na majirani zetu 60 walitia sahihi ili kuidhinisha ombi letu. Jirani mmoja alituambia hivi: “Hata ikiwa mtahitaji sahihi 200, mtapata.”
Wajenzi wawili wa Majumba ya Ufalme wenye uzoefu walikuja kusimamia ujenzi huo uliokamilika Novemba 2014. Hatukuwahi kufikiria kamwe kwamba kutaniko letu lingeweza kuwa na mahali bora pa ibada. Kwa kweli, Yehova ametubariki zaidi ya tulivyotarajia!