Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Umalizio

Umalizio

KUSUDI la broshua hii haikuwa kuzungumzia itikadi zote za kidini za Mashahidi wa Yehova. Badala ya hivyo, tumejitahidi kueleza baadhi ya kanuni ambazo Mashahidi huamini na kuonyesha wazi aina za uvutano mbalimbali wa familia unaoathiri mwanafunzi wako ikiwa mzazi mmoja au wote wawili ni Mashahidi.

Mashahidi wa Yehova hukazia sana ukuzi wa kiroho wa watoto wao. Nao wahisi uhakika kwamba huo huendeleza ukuzi wa watoto wao katika mambo mengine. Itikadi wanazokubali na kanuni wanazofuata huzipa maisha zao maana nazo huwasaidia washughulike na matatizo yao ya kila siku. Kwa kuongezea, itikadi na kanuni hizo zapasa kuwasukuma wajaribu kuwa wanafunzi wenye bidii na raia wema muda wote wa maisha.

Mashahidi hujitahidi kuona maisha kihalisi, kwa hiyo wao huiona elimu kuwa ya maana sana. Kwa hiyo, ni tamaa yao kushirikiana nawe kwa uwezo wao wote. Kwa upande wao, wakiwa nyumbani mwao na katika mahali pao mbalimbali pa ibada kotekote ulimwenguni, wao wataendelea kuwatia moyo watoto wao watimize daraka lao katika ushirikiano huu wenye matokeo.