Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mfano wa Kuigwa—Hezekia

Mfano wa Kuigwa—Hezekia

Mfano wa Kuigwa—Hezekia

Hezekia anakabili uamuzi mzito. Akiwa na umri wa miaka 25 tu, tayari ni mfalme wa Yuda. Atakuwa mfalme wa aina gani? Je, ataruhusu mfano mbaya wa baba yake, Mfalme Ahazi, umwathiri? Ahazi alikuwa mwasi-imani asiyetubu mpaka alipokufa. Aliendeleza ibada ya kipagani, na hata akateketeza angalau mmoja wa ndugu za Hezekia kwenye madhabahu ya kipagani. (2 Mambo ya Nyakati 28:1-4) Hata hivyo, Hezekia haruhusu mwenendo wenye unafiki wa baba yake umfanye achukizwe na ibada ya Yehova, wala haamini kwamba mtoto wa nyoka ni nyoka. Badala yake, Hezekia anaendelea “kushikamana na Yehova.”2 Wafalme 18:6.

Je, mmoja wa wazazi wako anadhihaki ibada ya Yehova? Je, ni mkatili au ana mazoea fulani yasiyofaa? Ikiwa ndivyo, si lazima uwe kama mzazi wako! Hezekia hakuruhusu hali mbaya ya familia yao iharibu maisha yake. Alikuwa mfalme mzuri sana hivi kwamba “baada yake hapakuwa na yeyote kama yeye kati ya wafalme wote wa Yuda.” (2 Wafalme 18:5) Kama Hezekia, wewe pia unaweza kufanikiwa maishani mwako hata ikiwa kuna hali ngumu katika familia yenu. Jinsi gani? Kwa kuendelea “kushikamana na Yehova.”