Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 2

Mungu Ndiye Rafiki Bora Uwezaye Kuwa Naye

Mungu Ndiye Rafiki Bora Uwezaye Kuwa Naye

Kuwa rafiki ya Mungu ndilo jambo bora zaidi kwako. Mungu atakufundisha jinsi ya kuwa mwenye furaha na mwenye usalama; atakuweka huru kutokana na imani nyingi zisizo za kweli na mazoea yanayodhuru. Atasikiliza sala zako. Atakusaidia ufurahie amani ya ndani na uwe na uhakika. (Zaburi 71:5; 73:28) Mungu atakusaidia wakati wa matatizo. (Zaburi 18:18) Na Mungu anakutolea zawadi yake ya uhai udumuo milele.—Waroma 6:23.

Umkaribiapo Mungu, utawakaribia rafiki za Mungu. Wao watakuwa rafiki zako pia. Kwa kweli, watakuwa kama ndugu na dada zako. Watafurahia kukufundisha juu ya Mungu nao watakusaidia na kukutia moyo.

Sisi hatulingani na Mungu. Unapojitahidi kuwa rafiki ya Mungu, lazima uelewe jambo moja muhimu. Kuwa rafiki ya Mungu si sawa na kuwa rafiki ya mtu mnayelingana. Mungu ni wa kale zaidi na mwenye hekima zaidi, naye ana nguvu zaidi kuliko sisi. Yeye ndiye Mtawala aliye na haki ya kututawala. Basi tukitaka kuwa rafiki zake, ni lazima tumsikilize na kufanya mambo anayotuambia tufanye. Tukifanya hivyo, tutapata mema sikuzote.—Isaya 48:18.