SOMO LA 16
Onyesha Upendo Wako Kwa Mungu
Ili uendelee kuwa na rafiki, wahitaji kuzungumza naye. Wewe humsikiliza, naye hukusikiliza. Pia wewe huwaambia watu wengine mambo mema juu ya rafiki yako. Hali iko hivyo kuhusiana na kuwa rafiki ya Mungu. Fikiria mambo ambayo Biblia inasema kuhusu hilo:
Zungumza na Yehova kwa ukawaida katika sala. “Dumuni katika sala.”—Waroma 12:12.
Soma Neno la Mungu, Biblia. “Andiko lote limepuliziwa na Mungu na ni lenye manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo.”—2 Timotheo 3:16.
Wafundishe wengine juu ya Mungu. “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . [mkiwafundisha] kushika mambo yote ambayo mimi nimewaamuru nyinyi.”—Mathayo 28:19, 20.
Hudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme. “Acheni tufikiriane ili kuchocheana kwenye upendo na kazi zilizo bora, . . . [tukitiana] moyo.”—Waebrania 10:24, 25.
Unga mkono kazi ya Ufalme. “Acheni kila mmoja [atoe] kama vile ameazimia moyoni mwake, si kwa kinyongo au kwa shurutisho, kwa maana Mungu hupenda mpaji mchangamfu.”—2 Wakorintho 9:7.