Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 7

Onyo la Wakati Uliopita

Onyo la Wakati Uliopita

Yehova hataruhusu watu wabaya waiharibu Paradiso. Rafiki zake peke yao ndio watakaoishi humo. Ni nini kitakachowapata watu wabaya? Ili upate jibu, fikiria kisa halisi cha Noa. Noa aliishi maelfu ya miaka iliyopita. Alikuwa mtu mzuri ambaye sikuzote alijitahidi kufanya mapenzi ya Yehova. Lakini watu wale wengine duniani walifanya mambo mabaya. Basi, Yehova akamwambia Noa kwamba Angeleta furiko ili awaharibu watu wote hao waliokuwa waovu. Alimwambia Noa ajenge safina ili yeye na familia yake wasife wakati ambapo Furiko lingekuja.—Mwanzo 6:9-18.

Noa na familia yake walijenga safina. Noa aliwaonya watu kwamba Furiko linakuja, lakini hawakumsikiliza. Waliendelea kufanya mambo mabaya. Baada ya safina kujengwa, Noa aliwaingiza wanyama ndani ya safina hiyo, naye pamoja na familia yake wakaingia ndani. Kisha Yehova akaleta mvua kubwa. Mvua hiyo ilinyesha siku 40, mchana na usiku. Maji yalijaa dunia yote.—Mwanzo 7:7-12.

Watu waovu walipoteza uhai wao, lakini Noa na familia yake wakaokolewa. Yehova aliwapitisha salama katika Furiko naye akawaweka katika dunia iliyosafishwa na kuondolewa uovu. (Mwanzo 7:22, 23) Biblia yasema kwamba wakati unakuja ambapo Yehova atawaharibu tena watu wanaokataa kufanya mambo mema. Watu wema hawataharibiwa. Wataishi milele katika dunia Paradiso.—2 Petro 2:5, 6, 9.

Leo watu wengi hufanya mambo mabaya. Ulimwengu umejaa matatizo. Yehova huwatuma Mashahidi wake tena na tena ili wawaonye watu, lakini watu wengi hawataki kuyasikiliza maneno ya Yehova. Hawataki kubadili njia zao. Hawataki kukubali yale ambayo Mungu anasema kuhusu mabaya na mema. Ni nini kitakachowapata watu hao? Je, siku moja watabadilika? Wengi wao hawatabadilika. Wakati unakuja ambapo watu waovu wataharibiwa nao hawataishi tena kamwe.—Zaburi 92:7.

Dunia haitaharibiwa; itafanywa paradiso. Wale wanaokuwa rafiki za Mungu wataishi milele katika Paradiso hiyo duniani.—Zaburi 37:29.