Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 9

Rafiki za Mungu Ni Nani?

Rafiki za Mungu Ni Nani?

Yesu Kristo ni Mwana wa Yehova, naye ndiye rafiki yake wa karibu zaidi na anayependwa zaidi. Kabla ya Yesu kuishi duniani akiwa mwanadamu, aliishi mbinguni akiwa kiumbe cha roho chenye uweza. (Yohana 17:5) Kisha akaja duniani kuwafundisha watu kweli juu ya Mungu. (Yohana 18:37) Pia alitoa uhai wake wa kibinadamu ili awaokoe wanadamu watiifu kutoka katika dhambi na kifo. (Waroma 6:23) Sasa Yesu ndiye Mfalme wa Ufalme wa Mungu, serikali ya mbinguni ambayo italeta Paradiso hapa duniani.—Ufunuo 19:16.

Malaika ni rafiki za Mungu pia. Malaika hawakuanza uhai wao hapa duniani wakiwa wanadamu. Waliumbiwa huko mbinguni kabla ya Mungu kuiumba dunia. (Ayubu 38:4-7) Kuna mamilioni ya malaika. (Danieli 7:10) Hao rafiki za Mungu wanaoishi mbinguni wanataka wanadamu wajifunze kweli juu ya Yehova.—Ufunuo 14:6, 7.

Mungu ana rafiki duniani pia; yeye huwaita mashahidi wake. Shahidi aliye mahakamani husema mambo anayojua kuhusu mtu au kitu fulani. Mashahidi wa Yehova huwaambia watu wengine mambo wanayojua juu ya Yehova na kusudi lake. (Isaya 43:10) Kama vile malaika, Mashahidi wanataka kukusaidia wewe ujifunze kweli juu ya Yehova. Wanataka wewe pia uwe rafiki ya Mungu.