Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 3

Unahitaji Kujifunza Juu ya Mungu

Unahitaji Kujifunza Juu ya Mungu

Ili uwe rafiki ya Mungu, unahitaji kujifunza juu yake. Je, rafiki zako wanajua jina lako, nao hulitumia? Ndiyo. Mungu pia akutaka ujue jina lake na kulitumia. Jina la Mungu ni Yehova. (Zaburi 83:18; Mathayo 6:9) Lazima pia ujifunze mambo yanayompendeza na yale yasiyompendeza. Unahitaji kujua rafiki zake na adui zake. Kumjua mtu huchukua muda. Biblia inasema kwamba inafaa kutenga wakati wa kujifunza juu ya Yehova.—Waefeso 5:15, 16.

Rafiki za Mungu hufanya mambo yanayompendeza. Wafikirie rafiki zako. Ukiwatendea mabaya na kufanya mambo wanayochukia, je, wataendelea kuwa rafiki zako? La, hasha! Vivyo hivyo, ukitaka kuwa rafiki ya Mungu, unahitaji kufanya mambo yanayompendeza.—Yohana 4:24.

Si dini zote hutokeza urafiki na Mungu. Yesu, ambaye ndiye rafiki wa karibu zaidi wa Mungu, alizungumza juu ya barabara mbili. Barabara moja ni pana nayo imejaa watu. Barabara hiyo huongoza kwenye uharibifu. Barabara ile nyingine ni nyembamba nayo ina watu wachache wanaoitembea. Barabara hiyo huongoza kwenye uhai udumuo milele. Kwa hiyo, ukitaka kuwa rafiki ya Mungu, lazima ujifunze njia ya kweli ya kumwabudu.—Mathayo 7:13, 14.