Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi

Utangulizi

MUNGU MWEZA YOTE ndiye Bwana wa ulimwengu wote. Uhai wetu wa sasa na wa wakati ujao unamtegemea. Ana uwezo wa kuthawabisha na uwezo wa kuadhibu. Ana uwezo wa kutupatia uhai na uwezo wa kuuondoa uhai. Tukipata kibali chake, tutafaidika; lakini tukikosa kibali chake, tutapatwa na mabaya. Basi, ni muhimu kama nini kwamba ibada yetu ikubalike kwake!

Watu huabudu katika njia mbalimbali. Ikiwa dini ni kama barabara, je, barabara zote za kidini zinakubaliwa na Mungu? La, sivyo. Yesu, nabii wa Mungu, alionyesha kwamba kuna barabara mbili tu. Alisema: “Ni pana na yenye nafasi barabara inayoongoza kuingia katika uharibifu, na wengi ndio wanaoingia kupitia hiyo; lakini lango ni jembamba na barabara ni yenye kufinyana inayoongoza kuingia katika uhai, na wachache ndio wanaoipata.”—Mathayo 7:13, 14.

Kuna dini aina mbili tu: moja inayoongoza watu kwenye uhai na nyingine inayowaongoza kwenye uharibifu. Kusudi la broshua hii ni kukusaidia uitambue barabara inayoongoza kwenye uhai wa milele.