Utangulizi wa Sehemu ya 11
Sehemu hii inaeleza kuhusu matukio yaliyo katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Yesu alizaliwa katika familia ya hali ya chini na waliishi katika mji mdogo. Alifanya kazi pamoja na baba yake, ambaye alikuwa seremala. Yesu ndiye angekuja kuwaokoa wanadamu. Yehova alikuwa amemchagua kuwa Mfalme wa Ufalme wa mbinguni. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako athamini jinsi Yehova alivyochagua kwa uangalifu familia na mazingira ambayo Yesu angelelewa. Fikiria jinsi Yehova alivyomlinda Yesu asiuawe na Herode na kwamba hakuna chochote kinachoweza kuzuia kusudi la Yehova. Jifunze jinsi Yehova alivyompa Yohana mgawo wa kutayarisha njia kwa ajili ya Yesu. Kazia jinsi Yesu alivyoonyesha kwamba alipenda hekima ya Yehova tangu alipokuwa mdogo.
KATIKA SEHEMU HII
Elisabeti Apata Mtoto
Kwa nini mume wa Elisabeti aliambiwa kwamba hangeweza kuzungumza mpaka mtoto azaliwe?
Gabrieli Amtembelea Maria
Alimpa ujumbe uliobadili maisha yake.
Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu
Wachungaji waliosikia tangazo hilo walichukua hatua haraka.
Yehova Alimlinda Yesu
Mfalme mwovu alitaka kumwua Yesu.
Yesu Akiwa Kijana
Ni kwa njia gani Yesu aliwashangaza walimu hekaluni?
Yohana Anatayarisha Njia
Yohana anakuwa nabii anapokuwa mtu mzima. Anafundisha kwamba Masihi anakuja. Watu wanaitikiaje ujumbe wake?