Utangulizi wa Sehemu ya 4
Katika sehemu hii tutajifunza kuhusu Yosefu, Ayubu, Musa, na Waisraeli. Wote walivumilia mambo mengi mabaya kutoka kwa Ibilisi. Baadhi yao walitendewa isivyo haki, wakafungwa gerezani, wakawa watumwa, na hata wengine wakauawa. Hata hivyo, Yehova aliwalinda katika njia mbalimbali. Ikiwa wewe ni mzazi, msaidie mtoto wako aelewe jinsi ambavyo watumishi hao wa Yehova walivumilia mambo mabaya bila kuruhusu imani yao idhoofike.
Yehova alileta Mapigo Kumi ili kuonyesha yeye ni mwenye nguvu kuliko miungu yote ya Wamisri. Kazia jinsi ambavyo Yehova aliwalinda watu wake wakati uliopita na jinsi anavyofanya hivyo leo.
KATIKA SEHEMU HII
Mtumwa Aliyemtii Mungu
Yosefu alifanya mambo mazuri, lakini bado aliteseka sana. Kwa nini?
Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe
Ingawa Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimthibitishia kwamba alikuwa pamoja naye.
Ayubu Alikuwa Nani?
Alimtii Yehova hata ilipokuwa vigumu.
Musa Aliamua Kumwabudu Yehova
Alipokuwa mtoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.
Mti Unaowaka Moto
Kwa nini moto haukuuteketeza mti huo?
Mapigo Matatu ya Kwanza
Farao aliwasababishia watu wake msiba kwa sababu kiburi kilimzuia achukue hatua moja tu rahisi.
Mapigo Sita Yaliyofuata
Mapigo hayo yalitofautianaje na mapigo matatu ya kwanza?
Pigo la Kumi
Pigo la mwisho lilikuwa baya sana hivi kwamba hata Farao mwenye kiburi alikubali mwishowe kuwaruhusu Waisraeli waondoke.
Muujiza Katika Bahari Nyekundu
Farao aliokoka mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?