Utangulizi wa Sehemu ya 9
Sehemu hii inatufundisha kuhusu vijana, manabii, na wafalme walioonyesha imani katika Yehova. Kule Siria, msichana mdogo Mwisraeli alikuwa na imani kwamba nabii wa Yehova angemponya Naamani. Nabii Elisha alikuwa na uhakika kwamba Yehova angemlinda kutokana na jeshi adui. Kuhani Mkuu Yehoyada alihatarisha uhai wake ili kumlinda Yehoashi, aliyekuwa bado mtoto, kutokana na nyanya (au bibi) yake mwovu, Athalia. Mfalme Hezekia alikuwa na uhakika kwamba Yehova ataiokoa Yerusalemu, na hata alipotishwa na Waashuru hakusalimu amri. Mfalme Yosia aliondoa kabisa ibada ya sanamu katika nchi yote, akarekebisha hekalu, na akarudisha ibada ya kweli nchini.
KATIKA SEHEMU HII
Shujaa na Msichana Mdogo
Msichana Mwisraeli alimweleza mke wa bwana mkubwa wake kuhusu nguvu za Yehova, naye Naamani akaponywa kimuujiza.
Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
Jinsi mtumishi wa Elisha alivyoona kwamba ‘kuna wengi walio pamoja nasi kuliko wale walio pamoja nao.’
Ujasiri wa Yehoyada
Kuhani mwaminifu anampinga kuhani mwovu.
Yehova Alimwonyesha Yona Subira
Ni jambo gani lililofanya nabii mmoja wa Mungu amezwe na samaki mkubwa? Alitokaje katika samaki huyo? Na Yehova alimfundisha jambo gani?
Malaika wa Yehova Alimlinda Hezekia
Maadui wa Yuda wanasema kwamba Yehova hatawalinda watu wake, lakini wamekosea!
Yosia Aliipenda Sheria ya Mungu
Yosia anaanza kutawala akiwa na umri wa miaka nane, naye anawasaidia watu wake kumwabudu Yehova.