Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mambo Makuu ya Sehemu ya 4

Mambo Makuu ya Sehemu ya 4

Zungumzia maswali yafuatayo pamoja na mwalimu wako:

  1. Soma Methali 13:20.

    • Kwa nini ni muhimu kuchagua marafiki wako kwa hekima?

      (Ona Somo la 48.)

  2. Ni ushauri gani wa Biblia unaoweza kukusaidia ikiwa wewe ni . . .

  3. Ni mazungumzo ya aina gani yanayomfurahisha Yehova? Ni mazungumzo ya aina gani ambayo hayamfurahishi Yehova?

    (Ona Somo la 51.)

  4. Ni kanuni gani za Biblia ambazo zitakusaidia kufanya maamuzi mazuri kuhusu mwonekano wako?

    (Ona Somo la 52.)

  5. Unawezaje kuchagua burudani inayomfurahisha Yehova?

    (Ona Somo la 53.)

  6. Soma Mathayo 24:45-47.

    • “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ni nani?

      (Ona Somo la 54.)

  7. Unawezaje kuunga mkono kutaniko kwa kutumia muda, nguvu, na mali zako?

    (Ona Somo la 55.)

  8. Soma Zaburi 133:1.

    • Unaweza kuchangia umoja katika kutaniko kupitia njia gani?

      (Ona Somo la 56.)

  9. Tunawezaje kupokea msaada wa Yehova ikiwa tutatenda dhambi nzito?

    (Ona Somo la 57.)

  10. Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9 na maelezo ya chini.

    • Unawezaje kuonyesha kwamba ‘umejitoa kikamili’ kwa Yehova wengine wanapopinga ibada ya kweli au wanapoacha kweli?

    • Je, unahitaji kufanya mabadiliko yoyote ili uendelee kuwa mshikamanifu kwa Yehova na kujitenga na dini ya uwongo?

      (Ona Somo la 58.)

  11. Unawezaje kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

    (Ona Somo la 59.)

  12. Unapanga kufanya nini ili uendelee kuimarisha urafiki wako na Yehova?

    (Ona Somo la 60.)