Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 2

Gharika Mpaka Kukombolewa Katika Misri

Gharika Mpaka Kukombolewa Katika Misri

Watu wanane peke yao ndio waliookoka Gharika, lakini baadaye wakaongezeka kuwa maelfu mengi. Kisha, ilipopita miaka 352 baada ya Gharika, Abrahamu akazaliwa. Tunajifuzna namna Mungu alivyotimiza ahadi yake kwa kumpa Abrahamu mwana anayeitwa Isaka. Kisha, kati ya wana wawili wa Isaka, Yakobo alichaguliwa na Mungu.

Yakobo alikuwa na jamaa kubwa ya wana 12 na binti fulani. Wana 10 wa Yakobo walimchukia ndugu yao mdogo Yusufu wakamwuza utumwani huko misri. Baadaye, Yusufu akawa mtawala mkuu wa Misri. Njaa kuu ilipotokea, Yusufu aliwajaribu ndugu zake aone kama wamegeuza moyo. Halafu, jamaa yote ya Yakobo, yaani, Waisraeli, wakahamia Misri. Hayo yalitokea miaka 290 baada ya kuzaliwa Abrahamu.

Kwa miaka 215 iliyofuata Waisraeli walikaa huko Misri. Yusufu alipokufa, wakawa watumwa huko. Mwishowe, Musa akazaliwa, naye Mungu akamtumia awakomboe Waisraeli kutoka Misri. Kwa jumla, miaka 857 ya historia inazungumziwa katika Sehemu ya 2.

 

KATIKA SEHEMU HII

HADITHI YA 11

Upinde wa Mvua wa Kwanza

Unapoona upinde wa mvua, unapaswa kukumbuka nini?

HADITHI YA 12

Watu Wanajenga Mnara Mkubwa

Mungu hakupendezwa, na adhabu aliyotoa bado huwaathiri wanadamu hadi leo.

HADITHI YA 13

Ibrahimu​—Rafiki ya Mungu

Kwa nini Ibrahimu aliacha makao yake ya starehe na kuanza kuishi katika mahema?

HADITHI YA 14

Mungu Anajaribu Imani ya Ibrahimu

Kwa nini Mungu alimwomba Ibrahimu amtoe mwana wake Isaka kuwa dhabihu?

HADITHI YA  15

Mke wa Lutu Alitazama Nyuma

Kile alichofanya kinatufundisha somo muhimu.

HADITHI YA 16

Isaka Anapata Mke Mzuri

Ni nini kilichofanya Rebeka awe mke mzuri? Je, ni urembo au ni jambo lingine?

HADITHI YA 17

Mapacha Waliokuwa Tofauti

Baba yao, Isaka, alimpenda sana Esau, lakini mama yao Rebeka, alimpenda sana Yakobo.

HADITHI 18

Yakobo Anakwenda Harani

Yakobo alimwoa Lea kwanza ingawa alimpenda sana Raheli.

HADITHI YA 19

Yakobo Ana Jamaa Kubwa

Je, majina ya makabila 12 ya Israeli yalitokana na wana 12 wa Yakobo?

HADITHI YA 20

Dina Anaingia Katika Taabu

Yote yalisababishwa na kuchagua marafiki wasiofaa.

HADITHI YA 21

Yusufu Anachukiwa na Ndugu Zake

Ni nini kiliwachochea baadhi yao watake kumuua ndugu yao?

HADITHI YA 22

Yusufu Anawekwa Katika Gereza

Afungwa gerezani, si kwa sababu alivunja sheria, lakini kwa sababu alifanya yaliyo sawa.

HADITHI YA 23

Ndoto za Farao

Kuna ufanani kati ya ng’ombe saba na masuke saba ya nafaka.

HADITHI YA 24

Yusufu Anajaribu Ndugu Zake

Atajuaje ikiwa wamebadilika tangu walipomuuza kama mtumwa?

HADITHI YA 25

Jamaa Inahamia Misri

Kwa nini familia ya Yakobo inaitwa Waisraeli na si Wayakobo?

HADITHI YA 26

Ayubu ni Mwaminifu kwa Mungu

Ayubu alipoteza mali, afya, na watoto. Je, Mungu alikuwa akimwadhibu?

HADITHI YA  27

Mfalme Mbaya Anatawala Misri

Kwa nini aliamuru watu wake wawaue watoto wote wa kiume wa Waisraeli?

HADITHI YA  28

Namna Mtoto Musa Alivyookolewa

Mama yake alitafuta njia ya kukwepa amri iliyoamuru watoto wavulana wa Waisraeli wauawe.

HADITHI YA  29

Sababu Musa Alikimbia

Musa alifikiria kwamba alikuwa tayari kuwaokoa Waisraeli alipokuwa na umri wa miaka 40, lakini hakuwa tayari.

HADITHI YA  30

Mti Mdogo Unaowaka

Kwa kutumia mfuatano wa miujiza, Mungu anamwambia Musa muda umefika wa Musa kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri.

HADITHI YA 31

Musa na Haruni Wanamwona Farao

Kwa nini Farao hamsikilizi Musa na kuwaachilia Waisraeli?

HADITHI YA 32

Mapigo 10

Mungu alileta mapigo kumi kwa sababu Farao, mtawala wa Misri kwa kiburi aliwakataza Waisraeli wasiondoke.

HADITHI YA 33

Kuvuka Bahari Nyekundu

Musa atenganisha Bahari Nyekundu kwa nguvu za Mungu na Waisraeli wavuka na kwenda nchi kavu.