Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 53

Ahadi ya Yeftha

Ahadi ya Yeftha

UMEPATA kutoa zawadi ukaona vigumu kuitimiza? Mwanamume katika picha hii, alitoa ahadi, ndiyo sababu ana huzuni sana. Huyo ni Yeftha, mwamuzi hodari wa Israeli.

Yeftha anakaa wakati Waisraeli hawamwabudu Yehova tena. Wanafanya mabaya tena. Yehova anaruhusu Waamoni wawaumize. Hilo lawafanya Waisraeli wamlilie Yehova hivi: ‘Tumekukosea. Tafadhali, utuokoe!’

Watu wanatubu mabaya waliyofanya. Wanaonyesha kutubu kwao kwa kumwabudu Yehova tena. Yehova anawasaidia tena.

Yeftha anachaguliwa na watu akapigane na Waamoni wabaya. Yeftha anataka sana Yehova amsaidie vitani. Basi anamwahidi Yehova hivi: ‘Ikiwa utanisaidia nishinde Waamoni, mtu wa kwanza kutoka nyumbani mwangu kuja kunilaki nirudipo nitakupa huyo.’

Yehova anasikiliza ahadi ya Yeftha, naye anamsaidia kushinda. Yeftha anaporudi nyumbani, unajua nani wa kwanza kutoka amlaki? Ni binti yake, mtoto wake mmoja tu. ‘O-o, binti yangu!’ Yeftha analia. ‘Unanihuzunisha sana. Lakini nimemwahidi Yehova, siwezi kuvunja ahadi hiyo.’

Binti Yeftha anapojua ahadi ya baba yake, kwanza anahuzunika. Maana ataacha baba na rafiki zake. Lakini atatumia maisha yake akimtumikia Yehova katika hema yake huko Shilo. Basi anamwambia baba yake hivi: ‘Ikiwa umemwahidi Yehova, timiza.’

Basi binti Yeftha aenda Shilo, na anamtumikia Yehova maisha yake yote katika hekalu lake. Kila mwaka wanawake wa Israeli wanamtembelea huko siku nne, na kufurahi pamoja. Watu wanampenda binti Yeftha kwa sababu ni mtumishi mzuri wa Yehova.