Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 36

Ndama ya Dhahabu

Ndama ya Dhahabu

MAMA WEE! Sasa watu wanafanya nini? Wanaabudu ndama! Kwa nini wanafanya hivyo?

Musa anapokawia mlimani, watu wasema hivi: ‘Hatujui yaliyompata Musa. Basi na tufanye mungu atutoe katika nchi hii.’

‘Vema,’ Haruni ndugu yake Musa asema. ‘Vueni pete zenu za dhahabu masikioni mniletee.’ Haruni anaziyeyusha na kufanya ndama ya dhahabu. Kisha watu wasema hivi: ‘Huyu ni Mungu wetu, aliyetutoa katika Misri!’ Halafu Waisraeli wanafanya karamu kubwa, na kuiabudu ndama hiyo ya dhahabu.

Yehova anapoona hayo, anakasirika sana. Anamwambia Musa hivi: ‘Fanya haraka ushuke. Watu wanafanya vibaya sana. Wamesahau sheria zangu nao wanaabudu ndama ya dhahabu.’

Musa anashuka haraka mlimani. Anapokaribia, anaona hivi. Watu wanaimba na kucheza wakizunguka ndama ya dhahabu! Musa anakasirika sana hata anayatupa chini mabamba mawili ya mawe yenye kuandikwa sheria, nayo yanavunjika-vunjika. Kisha anachukua ndama ya dhahabu na kuiyeyusha kabisa. Halafu anaisaga kuwa unga.

Watu wamefanya jambo baya sana. Musa anawaambia wanaume kati yao wachukue panga zao. ‘Wale watu wabaya walioiabudu ndama ya dhahabu lazima wafe,’ Musa anasema. Basi wanaume hao wanawaua watu 3,000! Inatupasa tumwabudu Yehova pekee kuliko miungu ya uongo, sivyo?