Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 66

Yezebeli - Malkia Mbaya Sana

Yezebeli - Malkia Mbaya Sana

BAADA ya Mfalme Yeroboamu kufa, kila mfalme anayetawala ufalme wa kaskazini wa makabila 10 ya Israeli ni mbaya. Mfalme Ahabu ndiye mfalme mbaya sana kuliko wote. Unajua sababu? Sababu moja kubwa ni mke wake, Malkia mbaya sana Yezebeli.

Yezebeli si mwanamke Mwisraeli. Ni binti ya mfalme wa Sidoni. Yezebeli anachukia Yehova tena anaua manabii wake wengi. Yezebeli akitaka kitu, anamwua mtu ili akipate.

Siku moja Mfalme Ahabu anahuzunika sana. Basi Yezebeli

anamwuliza hivi: ‘Kwa nini una huzuni leo?’

‘Kwa sababu ya maneno ya Nabothi,’ Ahabu anajibu. ‘Nilitaka kununua shamba lake la mizabibu. Lakini akakataa.’

‘Usihangaike,’ Yezebeli asema. ‘Nitakupatia.’

Basi Yezebeli anaandikia wakuu barua katika mji alimokuwa

akikaa mtu huyo Nabothi. ‘Waambieni watu wa ovyo-ovyo waseme kwamba Nabothi amemtukana Mungu na mfalme,’ anawaambia hivyo. ‘Kisha mmtoe Nabothi nje ya mji na kumpiga kwa mawe afe. ‘

Mara Yezebeli anapojua kwamba Nabothi amekufa, anamwambia Ahabu hivi: ‘Sasa nenda kachukue shamba lake.’ Yezebeli anapaswa kuadhibiwa kwa kufanya ubaya huo, sivyo?

Basi, wakati fulani, Yehova anamtuma Yehu akamwadhibu. Yezebeli anaposikia kwamba Yehu anakuja, anapaka macho yake rangi na kujipamba ili aonekane mrembo. Lakini Yehu anapokuja na kumwona Yezebeli katika dirisha, anawapazia sauti wanaume walio katika jumba la kifalme: ‘Mwangusheni chini!’ Wanaume hao wanatii, kama unavyowaona katika picha. Wanamwangusha chini, naye anakufa. Huo ndio mwisho wa Yezebeli Malkia mbaya sana.