Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 6

Kuzaliwa Yesu Mpaka Kufa Kwake

Kuzaliwa Yesu Mpaka Kufa Kwake

Malaika Gabrieli alitumwa kwa msichana mzuri jina lake Mariamu (Maria). Akamwambia ya kuwa angezaa mtoto ambaye angetawala milele akiwa mfalme. Mtoto huyo, Yesu, alizaliwa katika boma la ng’ombe, ambamo wachungaji walimtembelea. Baadaye, nyota ikaongoza watu kutoka Mashariki mpaka kwenye mtoto mchanga. Twajifunza aliyeonyesha nyota hiyo, na namna Yesu alivyookolewa asiuawe.

Halafu, Yesu akiwa mwenye miaka 12, twamwona akizungumza na waalimu katika hekalu. Miaka kumi na minane baadaye Yesu anabatizwa, kisha aanza kazi ya kuhubiri Ufalme na kufundisha ambayo Mungu alimtuma duniani aifanye. Ili wamsaidie kazi hiyo, Yesu alichagua wanaume 12 akawafanya mitume wake.

Pia Yesu alifanya miujiza mingi. Alilisha maelfu ya watu samaki wachache na mikate michache. Aliponya wagonjwa na hata kufufua wafu. Mwishowe, twajifunza mambo mengi yaliyompata Yesu siku ya mwisho ya kuishi kwake, na namna alivyouawa. Yesu alihubiri muda wa miaka mitatu na nusu, basi Sehemu ya 6 inazungumza kipindi cha miaka mingi kidogo kuliko 34.

 

KATIKA SEHEMU HII

HADITHI YA 84

Malaika Anatembelea Mariamu

Analeta ujumbe kutoka kwa Mungu: Mariamu atapata mtoto ambaye atakuwa mfalme milele.

HADITHI YA 85

Yesu Anazaliwa Katika Boma la Ng’ombe

Kwa nini mfalme anayekuja azaliwe mahali ambapo wanyama wanalishiwa?

HADITHI YA 86

Wanaume Walioongozwa na Nyota

Ni nani aliyewaongoza mamajusi kwa Yesu? Jibu linaweza kukushangaza.

HADITHI YA 87

Kijana Yesu Katika Hekalu

Ana mambo ambayo yanawashangaza hata watu wazima wanaofundisha katika hekalu.

HADITHI YA 88

Yohana Anambatiza Yesu

Yohana amekuwa akiwabatiza watenda dhambi, lakini Yesu hajatenda dhambi kamwe. Kwa nini Yohana alimbatiza?

HADITHI YA 89

Yesu Anasafisha Hekalu

Yesu anaonyesha aina ya upendo ambao unamsukuma kuwa na hasira.

HADITHI YA 90

Pamoja na Mwanamke Penye Kisima

Maji ambayo Yesu atampa yatawezaje kumfanya asione kiu tena kamwe?

HADITHI YA 91

Yesu Anafundisha Juu ya Mlima

|Jifunze hekima isiyopitwa na wakati kutoka katika Mahubiri ya Mlimani ya Yesu.

HADITHI YA 92

Yesu Anafufua Wafu

Kwa kutumia nguvu za Mungu, Yesu alisema maneno mawili rahisi na kumfufua binti ya Yairo.

HADITHI YA 93

Yesu Analisha Watu Wengi Chakula

Kwa kuwalisha maelfu ya watu kimuujiza, Yesu alithibitisha jambo gani muhimu?

HADITHI YA 94

Anapenda Watoto Wadogo

Yesu aliwafundisha mitume kwamba wana mengi ya kujifunza si tu kuhusu watoto wadogo bali pia kutoka kwa watoto wadogo.

HADITHI YA 95

Namna Yesu Anavyofundisha

Mfano wa Yesu wa jirani Msamaria ni mmoja kati ya mifano mingi inayoonyesha njia yake ya kufundisha aliyoitumia kwa ukawaida.

HADITHI YA 96

Yesu Anaponya Wagonjwa

Yesu anatimiza nini kupitia miujiza yote anayofanya?

HADITHI YA 97

Yesu Aja Kama Mfalme

Umati mkubwa unamkaribisha Yesu, lakini si wote wanaofurahishwa na jambo hilo.

HADITHI YA 98

Juu ya Mlima wa Mizeituni

Yesu aliwaambia mitume wake wanne mambo ambayo yanatukia katika siku zetu.

HADITHI YA 99

Katika Chumba cha Juu

Kwa nini Yesu anawaambia mitume wake waadhimishe mlo huu wa pekee kila mwaka?

HADITHI YA 100

Yesu Katika Bustani

Kwa nini Yuda alimsaliti Yesu kwa kumbusu?

HADITHI YA 101

Yesu Anauawa

Akiwa ametundikwa juu ya mti wa mateso, Yesu alitoa ahadi kuhusu paradiso.