Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 7

Kufufuliwa kwa Yesu Mpaka Kufungwa kwa Paulo

Kufufuliwa kwa Yesu Mpaka Kufungwa kwa Paulo

Siku ya tatu baada ya kufa kwake, Yesu alifufuliwa. Siku hiyo akaonekana kwa wafuasi wake mara tano zilizo tofauti. Yesu akaendelea kuonekana kwao kwa siku 40. Kisha, wengine kati ya wanafunzi wake walipokuwa wakitazama, Yesu akapanda mbinguni. Siku kumi baadaye Mungu alimwaga roho takatifu juu ya wafuasi wa Yesu waliokuwa wakingoja Yerusalemu.

Baadaye, adui za Mungu wakasababisha kufungwa kwa mitume gerezani, lakini malaika aliwafungua. Wapinzani walimpiga mwanafunzi Stefano kwa mawe akafa. Lakini twajifunza jinsi Yesu alivyomchagua mmoja wa wapinzani hao awe mtumishi wake wa pekee, akawa mtume Paulo. Ndipo, miaka mitatu na nusu baada ya kufa kwa Yesu, Mungu akamtuma mtume Petro akamhubiri Kornelio asiye Myahudi na jamaa yake.

Karibu miaka 13 baadaye Paulo alianza safari yake ya kuhubiri. Katika safari yake ya pili Timotheo ajiunga na Paulo. Twajifunza jinsi Paulo na wasafiri wenzake walivyoona mambo mengi ya kufurahisha katika kumtumikia Mungu. Mwishowe, Paulo akafungwa Roma. Miaka miwili baadaye akafunguliwa, lakini akafungwa tena na kuuawa. Matukio ya Sehemu ya 7 yalitukia kwa muda wa miaka kama 32.

 

KATIKA SEHEMU HII

HADITHI YA 102

Yesu Yuko Hai

Baada ya malaika kuliviringisha jiwe kutoka katika kaburi la Yesu, askari waliokuwa wakilinda walishtushwa na kile walichoona ndani ya kaburi.

HADITHI YA 103

Ndani ya Chumba Kilichofungwa

Kwa nini wanafunzi wake hawakumtambua baada Yesu ya kufufuliwa?

HADITHI YA 104

Yesu Anarudi Mbinguni

Kabla Yesu hajapaa angani, anawapa wanafunzi wake amri moja ya mwisho.

HADITHI YA 105

Kungojea Yerusalemu

Kwa nini Yesu aliwamwagia wanafunzi wake roho takatifu katika siku ya Pentekoste?

HADITHI YA 106

Wanafunguliwa Katika Gereza

Viongozi wa kidini Wayahudi wanawaweka mitume gerezani ili kusimamisha kazi yao ya kuhubiri, lakini Mungu ana mpango mwingine tofauti.

HADITHI YA 107

Stefano Anapigwa kwa Mawe

Alipokuwa akiuawa, Stefano alitoa sala ya pekee sana.

HADITHI YA 108

Wakienda Damasko

Mwangaza unaopofusha na sauti kutoka mbinguni vyabadili maisha ya Sauli.

HADITHI YA 109

Petro Anamtembelea Kornelio

Je Mungu anawaona watu kutoka jamii au taifa moja kuwa bora kuliko wale wa jamii au mataifa mengine?

HADITHI YA 110

Timotheo—Msaidizi Mpya wa Paulo

Timotheo anaondoka nyumbani na kujiunga na Paulo katika safari yenye kusisimua ya kuhubiri.

HADITHI YA 111

Mvulana Aliyelala Usingizi

Eutiko analala usingizi wakati wa hotuba ya kwanza ya Paulo, lakini si wakati wa hotuba ya pili. Kilichotukia katikati ya hotuba hizo ni, muujiza.

HADITHI YA 112

Meli Inaharibika Katika Kisiwa

Mara tu inapoonekana hakuna tumaini, Paulo anapokea ujumbe kutoka kwa Mungu unaompa matumaini.

HADITHI YA 113

Paulo Katika Roma

Paulo angewezaje kufanya kazi yake kama mtume huku akiwa mfungwa?