Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 104

Yesu Anarudi Mbinguni

Yesu Anarudi Mbinguni

WAKATI siku zinapopita, Yesu anajionyesha kwa wafuasi wake mara nyingi. Wakati mmoja wanafunzi kama 500 wanamwona. Anapowatokea, unajua Yesu anawaambia nini? Ufalme wa Mungu. Yehova alimtuma Yesu duniani afundishe habari za Ufalme huo. Anazidi kufanya hivyo hata baada ya kufufuliwa katika wafu.

Unakumbuka maana ya ufalme wa Mungu? Ufalme ni serikali halisi ya Mungu mbinguni, naye Yesu Ndiye Mungu amechagua awe mfalme. Kama tulivyokwisha jifunza, Yesu alionyesha atakavyokuwa mfalme mwema sana kwa kulisha wenye njaa chakula, kwa kuponya wagonjwa, hata kufufua wafu!

Basi, Yesu atakapotawala mbinguni kwa miaka elfu, dunia itakuwaje? Dunia yote itafanywa kuwa paradiso nzuri. Hakutakuwako vita tena, wala uvunjaji wa sheria, wala magonjwa, wala hata kifo. Twajua hayo ni ya kweli kwa sababu Mungu aliifanya dunia iwe paradiso watu wafurahie. Ndiyo maana aliifanya bustani ya Edeni mwanzoni. Naye Yesu atatimiza mapenzi ya Mungu.

Sasa wafika wakati wa Yesu kurudi mbinguni. Kwa muda wa siku 40 amekuwa akijionyesha kwa wanafunzi wake. Basi wana hakika kwamba yuko hai tena. Lakini kabla ya kuacha wanafunzi wake anawaambia hivi: ‘Kaeni Yerusalemu mpaka mpokee roho takatifu.’ Roho takatifu ni nguvu ya utendaji ya Mungu, ni kama upepo unaovuma, itakayosaidia wafuasi wake wafanye mapenzi ya Mungu. Mwishowe, anasema: ‘Mtahubiri habari zangu kwenye sehemu za mbali za dunia.’

Yesu akiisha kusema hivyo, ajabu yatokea. Anaanza kupanda mbinguni, kama unavyoona hapa. Ndipo wingu lamficha asionekane, na wanafunzi hawamwoni Yesu tena. Yesu anaenda mbinguni, na kuanza huko kutawala wanafunzi wake walio duniani.