Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HADITHI YA 115

Paradiso Mpya Duniani

Paradiso Mpya Duniani

TAZAMA miti ile mirefu, maua mazuri na milima mirefu. Je! hapa si pazuri? Angalia yule paa anavyokula katika mkono wa kivulana huyu. Watazame tena simba wale na farasi waliosimama pale katika shamba la majani. Ungependa kukaa katika nyumba mahali kama hapa?

Mungu anataka wewe ukae milele duniani katika paradiso. Hataki upate maumivu na uchungu unaosumbua watu leo. Biblia inaahidi hivi wale watakaokaa katika paradiso mpya: ‘Mungu atakuwa pamoja nao. Hakutakuwa tena kifo wala kulia wala maumivu. Mambo ya kale yamekwisha.’

Yesu atatokeza badiliko zuri hilo. Unajua litakea wakati gani? Baada ya kuondoa mabaya na waovu wote duniani. Kumbuka, Yesu alipokuwa hapa duniani aliponya watu magonjwa yote, hata akafufua wafu. Yesu alifanya hivyo ili aonyeshe atakavyofanya duniani pote akiwa Mfalme wa ufalme wa Mungu.

Ebu fikiri itakuwa vizuri kama nini katika paradiso mpya hapa duniani! Yesu, pamoja na wengine ambao anachagua, watakuwa wakitawala mbinguni. Watawala hao wataangalia wote duniani na kuhakikisha kwamba wanafurahi. Na tuone yanayotupasa kufanya ili tuhakikishe kwamba Mungu atatupa uzima wa milele katika paradiso yake mpya.