SEHEMU YA TATU
‘Nitawakusanya Pamoja’—Ahadi ya Kurudishwa kwa Ibada Safi
WAZO KUU: Unabii wa Ezekieli wafunua kurudishwa kwa ibada safi
Taifa la Israeli limesambaratika—halina umoja kwa sababu ya uasi imani. Linapatwa na matokeo ya matendo yake; lilichafua ibada safi na kuliletea suto jina la Mungu. Katika hali hiyo ya kusikitisha, Yehova anamchochea Ezekieli atoe mfululizo wa unabii unaoleta tumaini. Akitumia lugha ya mfano na maono yenye kustaajabisha, Yehova anawatia moyo mateka wa Israeli na wote wanaotamani kuona ibada safi ikirudishwa.
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 8
“Nitamweka Mchungaji Mmoja”
Mungu amwongoza Ezekieli aandike unabii kumhusu Masihi, Mtawala na Mchungaji wa wakati ujao wa watu wa Yehova, ambaye atarudisha ibada safi itakayodumu.
SURA YA 9
“Nitawapa Moyo Wenye Umoja”
Unabii uliotolewa kwa wahamishwa waaminifu Wayahudi huko Babiloni una maana gani kwetu?
SURA YA 10
“Mtakuwa Hai”
Ezekieli anaona maono ya bonde lililojaa mifupa mikavu ambayo inakuwa hai. Inamaanisha nini?
SURA YA 14
“Hii Ndiyo Sheria ya Hekalu”
Wayahudi walijifunza mambo gani kutokana na hekalu aliloona Ezekieli? Maono hayo yanatufundisha nini leo?