Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 2A

Kuuelewa Unabii wa Ezekieli

Kuuelewa Unabii wa Ezekieli

UFAFANUZI—UNABII NI NINI?

Katika Biblia, kitenzi cha Kiebrania na·vaʼʹ, kinachotafsiriwa “kutoa unabii,” humaanisha hasa kutangaza ujumbe ulioongozwa na roho ya Mungu, hukumu, mafundisho ya maadili, au amri kutoka kwa Mungu. Pia, linaweza kumaanisha kutoa tangazo linalotoka kwa Mungu kuhusu jambo litakalotokea. Unabii wa Ezekieli unahusisha aina hizo zote za ufunuo kutoka kwa Mungu.—Eze. 3:10, 11; 11:4-8; 14:6, 7; 37:9, 10; 38:1-4.

JINSI ULIVYOWASILISHWA

  • MAONO

  • MIFANO

  • VIELEZI

Kitabu cha Ezekieli kina maono, mifano, vielezi, na maigizo ya ujumbe wa unabii.

UTIMIZO

Nyakati nyingine unabii uliotolewa na Ezekieli una utimizo zaidi ya mmoja. Kwa mfano, unabii uliohusu kurudishwa kwa ibada safi ulitimizwa kwa kiwango kidogo watu wa Mungu waliporudi katika Nchi ya Ahadi. Lakini kama inavyozungumziwa katika Sura ya 9 ya kitabu hiki, unabii mwingi unaohusu kurudishwa kwa ibada safi unatimizwa leo na pia utatimizwa wakati ujao.

Wakati uliopita, tulifikiri kwamba sehemu nyingi za unabii wa Ezekieli zilikuwa na utimizo halisi na utimizo wa mfano. Hata hivyo, kitabu hiki hakisemi kwamba mtu, kitu, mahali, au tukio lolote ni ufananisho wa kinabii wa jambo fulani linalotimia siku zetu, isipokuwa kuwe na msingi wa Kimaandiko wa kufanya hivyo. * Badala yake, kitazungumzia utimizo mkubwa zaidi wa unabii wa Ezekieli. Pia, kitazungumzia masomo tunayojifunza kutokana na ujumbe wa Ezekieli na pia watu, maeneo, na matukio aliyotaja.

^ fu. 12 Kwa maelezo zaidi kuhusu maana halisi na maana ya mfano (ufananisho), tazama gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2015, uku. 9-11, fu. 7-12; na “Maswali Kutoka kwa Wasomaji,” uku. 17-18 wa gazeti hilo.