Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 4A

‘Niliendelea Kuwatazama Viumbe Hai’

‘Niliendelea Kuwatazama Viumbe Hai’

Bila shaka, Ezekieli alikuwa ameona sanamu kubwa zilizochongwa za ng’ombe dume na simba wenye mabawa na vichwa vya binadamu mbele ya mahekalu na majumba ya kifalme. Sanamu kama hizo zilipatikana kotekote katika Ashuru la kale na Babilonia. Kama watazamaji wengine, bila shaka Ezekieli alistaajabu kuona sanamu hizo, baadhi yazo zilikuwa na urefu wa karibu mita 6. Hata hivyo, ingawa wanyama hao walionekana kuwa wenye nguvu, zilikuwa sanamu za mawe zisizo na uhai.

Tofauti na hilo, viumbe wanne ambao Ezekieli aliona katika maono walikuwa “viumbe hai.” Hiyo ni tofauti kubwa! Ezekieli alistaajabu kuona viumbe hao hivi kwamba katika mwanzo wa unabii wake anawataja “viumbe hai” mara 11. (Eze. 1:5-22) Maono ya wale viumbe hai wanne wanaosonga kwa pamoja chini ya kiti cha ufalme cha Mungu, yalimhakikishia kabisa Ezekieli kwamba Yehova ana uwezo kamili juu ya uumbaji wote. Leo, maono hayo yanatuhakikishia waziwazi ukuu na nguvu za Yehova na utukufu wa enzi yake kuu.—1 Nya. 29:11.