SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 13A
Mahekalu Tofauti, Masomo Tofauti
Hekalu Ambalo Ezekieli Aliona:
-
Ezekieli aliwafafanulia wahamishwa Wayahudi huko Babiloni kulihusu
-
Lina madhabahu ambapo dhabihu nyingi zinatolewa
-
Linakazia viwango vya Yehova vya uadilifu kuhusu ibada
-
Linakazia fikira zetu kwenye kurudishwa kwa ibada safi kulikoanza mwaka wa 1919
Hekalu Kubwa la Kiroho:
-
Paulo alilifafanua alipokuwa akiwaandikia Wakristo Waebrania
-
Lina madhabahu ambapo dhabihu moja inatolewa, “mara moja kwa wakati wote” (Ebr. 10:10)
-
Linafafanua uhalisi wa mpango wa kiroho ambao ulikaziwa zamani kupitia hema la ibada na mahekalu halisi—Mpango wa Yehova wa ibada safi kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Kristo
-
Linakazia fikira zetu kwenye kazi ambayo Kristo alifanya akiwa Kuhani Mkuu Zaidi kuanzia mwaka wa 29 hadi 33 W.K.