Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 7B

Maneno Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli

Maneno Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli

“Mwana wa Binadamu”

ZAIDI YA MARA 90

Ezekieli anaitwa “mwana wa binadamu” zaidi ya mara 90. (Eze. 2:1) Kwa hiyo, Yehova anamkumbusha kwamba ingawa alipata mapendeleo makubwa, yeye ni mwanadamu tu. Inapendeza kwamba katika masimulizi ya Injili, Yesu anaitwa “Mwana wa binadamu” mara 80, na hilo linaonyesha kwamba alikuwa mwanadamu kamili na si malaika aliyevaa mwili wa mwanadamu.—Mt. 8:20.

“. . . Mtalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

ZAIDI YA MARA 50

Zaidi ya mara 50, Ezekieli anaandika maneno ya Mungu kwamba watu watalazimika “kujua kwamba mimi ni Yehova,” na maneno hayo yanakazia kwamba ni Yehova peke yake anayestahili kupokea ibada safi.—Eze. 6:7.

“Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova”

MARA 217

Maneno “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova” yanapatikana mara 217, na hivyo kuonyesha umuhimu wa jina la Mungu na kukazia kwamba uumbaji wote uko chini ya Yehova.—Eze. 2:4.