Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 9D

Unabii Kuhusu Utekwa na Kurudishwa

Unabii Kuhusu Utekwa na Kurudishwa

Unabii mwingi kuhusu utekwa wa Wayahudi katika Babiloni la kale ulitimizwa kwa mara ya pili, kwa njia kubwa zaidi wakati wa utekwa wa baadaye wa kutaniko la Kikristo katika Babiloni Mkubwa. Hebu chunguza mifano kadhaa.

1. MAONYO

2. UTEKWA

3. KURUDISHWA

UTIMIZO WA KWANZA

Kabla ya mwaka wa 607 K.W.K.​—Isaya, Yeremia, na Ezekieli wawaonya watu wa Yehova; hata hivyo, bado uasi imani unasitawi

607 K.W.K.​—Yerusalemu laharibiwa; watu wa Mungu wapelekwa utekwani Babiloni

Mwaka wa 537 K.W.K. na kuendelea​—Watu wachache waaminifu waliobaki warudi Yerusalemu, wajenga hekalu, na kurudisha ibada safi

UTIMIZO MKUBWA ZAIDI

Karne ya Kwanza W.K.​—Yesu, Paulo, na Yohana waonya kutaniko, lakini bado uasi imani unasitawi

Kuanzia Karne ya Pili W.K.​—Wakristo wa kweli wapelekwa utekwani katika Babiloni Mkubwa

1919 W.K. na kuendelea​—Chini ya utawala wa Yesu, watiwa mafuta waaminifu waona mwisho wa uhamisho wao wa kiroho na kurudishwa kwa ibada safi