Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA PILI

“Mlipachafua Mahali Pangu Patakatifu”​—Ibada Safi Yachafuliwa

“Mlipachafua Mahali Pangu Patakatifu”​—Ibada Safi Yachafuliwa

EZEKIELI 5:11

WAZO KUU: Yuda na Yerusalemu wapotoka kiroho na kiadili

Yehova aliwapenda na kuwatunza Waisraeli wakiwa “mali iliyothaminiwa sana.” (Kut. 19:5, maelezo ya chini.) Lakini walimkosea Yehova heshima kwa kuabudu miungu ya uwongo katika hekalu lilelile lililokuwa na jina lake! Walimkasirisha Yehova na kumletea aibu. Kwa nini Waisraeli walipotoka sana? Tunajifunza nini kutokana na unabii wa Ezekieli kuhusu kuharibiwa kwa Yerusalemu? Na tunapata somo gani kutokana na jinsi Waisraeli walivyoshughulika na mataifa yaliyowazunguka?

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 5

‘Ona Mambo Maovu na Yenye Kuchukiza Wanayofanya’

Ezekieli anaona mambo yenye kushtua ambayo yanaonyesha jinsi taifa lote lilivyopotoka kiroho.

SURA YA 6

“Sasa Mwisho Umekufikia”

Maigizo ya kinabii ya Ezekieli yalitabiri hasira ya Yehova dhidi ya Yerusalemu.

SURA YA 7

Mataifa Yatalazimika “Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova”

Mataifa yaliyolichafua jina la Mungu na kuwatesa au kuwapotosha watu wake hayangeepuka matokeo ya matendo yao. Tunajifunza nini kutokana na jinsi Waisraeli walivyoshughulika na mataifa hayo?