Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Kwa wale wanaompenda Yehova Mungu na Neno lake, Biblia:

Yesu alisema: “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.” (Yohana 8:32) Wazia jinsi ulivyohisi ulipojifunza kweli ya Biblia kwa mara ya kwanza! Ulisisimuka kujua kwamba katika ulimwengu uliojaa uwongo, tunaweza kujifunza kweli.—2 Timotheo 3:1.

Yehova Mungu anataka tujue kweli. Na kwa sababu tunawapenda wengine, tunataka kuwaeleza kuihusu. Lakini mengi zaidi yanahusika ili kumtumikia Mungu kwa njia inayofaa. Lazima tufanye yote tuwezayo kuishi kwa njia inayowafaa Wakristo kwa sababu tunaheshimu sana kanuni za Yehova. Yesu alieleza njia muhimu ambayo tunaweza kumthibitishia Mungu kwamba tunampenda. Alisema hivi: “Mkishika amri zangu, mtakaa katika upendo wangu, kama vile ambavyo nimeshika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.”—Yohana 15:10.

Yesu anampenda sana Baba yake, naye hufanya kila kitu ambacho Baba yake anamtaka afanye. Tukimwiga Yesu kwa kuishi maisha yanayofaa, Yehova atatupenda na tutakuwa na furaha ya kweli. Kama Yesu alivyosema, ‘mkijua mambo haya, mtakuwa wenye furaha mkiyatenda.’—Yohana 13:17.

Ni tumaini letu kwamba kitabu hiki kitakusaidia kujifunza kuishi kupatana na kweli ya Biblia na kuwa rafiki ya Mungu. Tunasali kwamba utaendelea kukua katika upendo kwa Mungu na kudumu ‘katika upendo wa Mungu ili hatimaye upate uzima wa milele.’—Yuda 21.

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova