Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Habari kwa Wajumbe

Habari kwa Wajumbe

MKUTANO WA PEKEE

SHULE YA WAENEZA-INJILI WA UFALME Mapainia wenye umri kati ya miaka 23 na 65 ambao wangependa kupanua utumishi wao, wanaalikwa kwenye mkutano wa wanaopenda kuhudhuria Shule ya Waeneza-Injili wa Ufalme utakaofanywa Jumapili alasiri. Mtatangaziwa wakati na mahali ambapo mkutano huo utafanywa.

HABARI KWA WAHUDHURIAJI

WAKARIBISHAJI Wakaribishaji wamepewa mgawo wa kukusaidia. Tafadhali shirikiana nao kikamili kwa kufuata mwelekezo wanaotoa wanapowaelekeza watu kuhusu mahali pa kuegesha, kuhifadhi viti, na mambo mengine.

UBATIZO Kwa kawaida, viti kwa ajili ya wale watakaobatizwa vitawekwa katika sehemu iliyo mbele ya jukwaa, isipokuwa maagizo tofauti yatolewe. Watakaobatizwa wanapaswa kuketi kwenye viti hivyo kabla ya hotuba ya ubatizo kuanza siku ya Jumamosi asubuhi. Kila mmoja anapaswa kubeba taulo na mavazi yanayofaa kwa ajili ya ubatizo.

MICHANGO Pesa nyingi zimetumiwa ili kupata viti vya kutosha, mfumo wa sauti, vifaa vya kuonyesha video, na huduma nyingine nyingi ili tufurahie kusanyiko na kutusaidia tumkaribie Yehova. Michango yenu ya hiari husaidia kulipia gharama hizo na pia inategemeza kazi ya ulimwenguni pote. Masanduku ya michango ambayo yameandikwa waziwazi yanapatikana kotekote katika mahali pa kusanyiko. Michango yote inathaminiwa sana. Baraza Linaloongoza linawashukuru kwa michango ya ukarimu inayotegemeza kazi ya Ufalme.

HUDUMA YA KWANZA Tafadhali kumbukeni kwamba idara hii hushughulikia mambo ya DHARURA TU.

VILIVYOPOTEA NA KUPATIKANA Vitu vyote ambavyo havijulikani ni vya nani vinapaswa kupelekwa kwenye Idara ya Vilivyopotea na Kupatikana. Ikiwa umepoteza kitu chochote, nenda kwenye idara hii na ufafanue jinsi kilivyo. Watoto ambao wamepotea wanapaswa kupelekwa kwenye idara hii. Hata hivyo, ili kuepuka usumbufu usio wa lazima, tafadhali watunze watoto wako, na uwe karibu nao kila wakati.

VITI Tafadhali wafikirie wengine. Kumbuka kwamba unaweza kuhifadhi viti kwa ajili tu ya watu ambao unaishi nao katika nyumba moja, wale unaosafiri nao katika gari moja, au wanafunzi wako wa Biblia. Tafadhali usiweke vitu kwenye viti ambavyo humhifadhii mtu yeyote.

UTUMISHI WA KUJITOLEA Ikiwa ungependa kujitolea kufanya kazi kusanyikoni, tafadhali nenda kwenye Idara ya Habari na Utumishi wa Kujitolea

Kusanyiko limepangwa na Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova