Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 14

Kukazia Mambo Makuu

Kukazia Mambo Makuu

Waebrania 8:1

MUHTASARI: Wasaidie wasikilizaji wafuatane na hotuba yako, na uweke wazi jinsi kila jambo kuu linavyohusiana na kichwa kikuu na jambo unalotaka kufundisha.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Uwe na lengo. Jiulize, je, hotuba hii imekusudiwa kuwashauri, kuwasadikisha, au kuwachochea wasikilizaji? Kisha uitoe kulingana na kusudi lake. Hakikisha kila jambo kuu linazungumziwa kwa njia itakayokusaidia kutimiza lengo lako.

  • Kazia kichwa kikuu katika hotuba yako. Rejelea kichwa kikuu katika hotuba yako yote kwa kurudia maneno makuu ya kichwa hicho au kwa kutumia maneno yanayofanana na hayo.

  • Fanya mambo makuu yawe wazi na rahisi. Chagua mambo makuu yanayohusiana na kichwa kikuu tu na ambayo utaweza kuyatumia kufundisha kwa wakati uliopangiwa. Usiwe na mambo mengi makuu. Taja kila jambo kuu waziwazi. Baada ya kuzungumzia jambo moja tua kidogo kabla ya kuanza kuzungumzia jambo kuu linalofuata. Onyesha uhusiano uliopo kati ya jambo kuu ambalo umemaliza kuzungumzia na linalofuata.