Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 16

Uwe Mwenye Kujenga na Mwenye Kutia Moyo

Uwe Mwenye Kujenga na Mwenye Kutia Moyo

Ayubu 16:5

MUHTASARI: Kazia fikira mambo yanayoweza kuboresha hali na yanayowachochea wasikilizaji.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Uwe na mtazamo mzuri kuelekea wasikilizaji wako. Jikumbushe kwamba waabudu wenzako wanataka kumpendeza Yehova. Hata ukilazimika kutoa shauri, kwanza jitahidi kuwapongeza kutoka moyoni.

  • Usizungumzie sana matatizo. Zungumzia mambo yasiyopendeza ikiwa tu mambo hayo ni muhimu katika hotuba. Kwa ujumla, hotuba yako inapaswa kuwa yenye kutia moyo.

  • Tumia vizuri Neno la Mungu. Kazia kile ambacho Yehova amefanya, anachofanya, na atakachofanya kwa ajili ya wanadamu. Wachochee wasikilizaji wawe na tumaini na ujasiri.