Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 2

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

2 Wakorintho 2:17

MUHTASARI: Zungumza kwa njia ya kawaida inayoonyesha jinsi unavyohisi kuhusu habari unayozungumzia na kuwahusu wasikilizaji wako.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Sali na ujitayarishe vizuri. Sali ili upate msaada wa kukazia fikira ujumbe wako, si kuhusu wasiwasi unaohisi. Hakikisha mambo makuu unayohitaji kuwasilisha yako wazi akilini mwako. Eleza mawazo kwa maneno yako mwenyewe; usirudie tu kusema maneno yaliyochapishwa.

  • Zungumza kutoka moyoni. Fikiria kwa nini wasikilizaji wanahitaji kusikia ujumbe wako. Wakazie fikira. Kisha kupitia njia yako ya kusimama, ishara zako, na uso wako utaonyesha uchangamfu na urafiki.

  • Watazame wasikilizaji wako. Watazame wale unaoongea nao ikiwa desturi za kwenu zinaruhusu. Unapotoa hotuba, usipitishe tu macho kutoka upande mmoja hadi mwingine ukiwatazama watu wote wa ujumla, bali mtazame mtu mmoja, kisha mtazame mwingine.