Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 20

Umalizio Wenye Matokeo

Umalizio Wenye Matokeo

Mhubiri 12:13, 14

MUHTASARI: Katika maneno yako ya kumalizia, wachochee wasikilizaji wakubali na kutumia mambo waliyojifunza.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Husianisha umalizio na habari yote kwa ujumla. Taja tena au utumie maneno mengine kurudia mambo makuu na mada kuu ya habari yako.

  • Wachochee wasikilizaji. Waonyeshe wasikilizaji wanachohitaji kufanya, na uwape sababu za msingi za kufanya hivyo. Zungumza kwa njia inayoonyesha unasadiki jambo unalosema na kwamba ni muhimu.

  • Umalizio uwe rahisi na mfupi. Usianze kutaja mambo makuu mapya. Ukitumia maneno machache iwezekanavyo, wachochee kwa mara ya mwisho wachukue hatua.