Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 6

Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Yohana 10:33-36

MUHTASARI: Usisome tu andiko na kuanza kuzungumzia jambo linalofuata. Hakikisha wasikilizaji wako wanaona waziwazi uhusiano kati ya andiko ulilosoma na jambo unalokazia.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tenga maneno makuu. Baada ya kusoma andiko, onyesha wazi maneno yanayohusiana moja kwa moja na jambo kuu. Unaweza kufanya hivyo kwa kurudia maneno hayo au kwa kuuliza swali linalowafanya wasikilizaji watambulishe maneno makuu.

  • Kazia jambo kuu. Ikiwa kabla ya kusoma andiko ulieleza sababu ya kulisoma, eleza jinsi maneno makuu ya andiko hilo yanavyopatana na sababu hiyo.

  • Rahisisha matumizi ya andiko. Epuka kuzungumzia mambo ambayo hayasaidii kuonyesha wazi jambo kuu. Kwa kutegemea wasikilizaji wako wanajua nini tayari kuhusu habari hiyo, amua ni mambo mangapi ambayo lazima yatajwe ili matumizi yawe wazi na yaeleweke.