Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 7

Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Luka 1:3

MUHTASARI: Tumia habari zinazoaminika kuwasaidia wasikilizaji kufikia mkataa sahihi.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tegemea vyanzo vinavyoaminika. Tumia Neno la Mungu kutegemeza maneno yako, ukisoma moja kwa moja kutoka katika Biblia inapowezekana. Ikiwa unataja jambo la kisayansi, taarifa ya habari, jambo lililoonwa, au habari nyingine inayounga mkono jambo unalosema, chunguza mapema ikiwa chanzo hicho kinategemeka na ni cha karibuni zaidi.

  • Tumia marejeo vizuri. Eleza maandiko kupatana na muktadha wake, ujumbe mkuu wa Biblia, na machapisho ya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Unapotumia vyanzo ambavyo si vya kimaandiko, hakikisha kwamba unafanya hivyo kwa usahihi bila kubadili maana ya awali au kusema kitu kwa njia tofauti na kile ambacho mwandishi alikusudia.

  • Wasaidie wasikilizaji wafikirie uthibitisho huo. Baada ya kusoma andiko au rejeo fulani, waulize wasikilizaji maswali kwa busara au utoe mfano unaoonyesha jambo kuu ili kuwasaidia wasikilizaji wafikie mkataa.