Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 8

Mifano Inayofundisha

Mifano Inayofundisha

Mathayo 13:34, 35

MUHTASARI: Boresha ufundishaji wako kwa kutumia mifano rahisi inayowavutia wasikilizaji wako na kufundisha mambo muhimu.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Chagua mifano rahisi. Kama Yesu, tumia mambo ya kawaida kuelezea mambo muhimu, na mambo rahisi kuelezea mambo magumu. Usiongeze habari zisizohitajika ambazo zitafanya mfano uwe mgumu. Hakikisha kwamba kila sehemu ya mfano wako inahusiana kikweli na somo unalofundisha ili wasikilizaji wasikengeushwe na sehemu zisizopatana.

  • Fikiria mambo yatakayowanufaisha wasikilizaji wako. Chagua mifano inayohusisha utendaji na mapendezi ya wasikilizaji wako. Uwe mwangalifu mifano yako isiwaaibishe au kuwakasirisha.

  • Fundisha jambo kuu. Toa mifano inayohusiana na jambo kuu, si mambo madogo. Hakikisha kwamba wasikilizaji wako hawakumbuki tu mfano, bali pia wanakumbuka jambo unalofundisha.