Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 9

Kutumia Picha na Video Vizuri

Kutumia Picha na Video Vizuri

Mwanzo 15:5

MUHTASARI: Tumia picha na video ili kufanya mambo unayofundisha yawe wazi na yaeleweke kwa urahisi.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Chagua vielelezo vitakavyoboresha ufundishaji wako. Unapotoa hotuba unaweza kutumia picha, michoro, ramani, mpangilio wa matukio, au vielelezo vingine vya aina hiyo ili kuonyesha mambo makuu wala si mambo madogo-madogo. Katika huduma unaweza pia kutumia video ili kutimiza kusudi hilo. Wasaidie wasikilizaji wako wakumbuke si tu vielelezo ulivyotumia bali jambo kuu lililofanya utumie vielelezo hivyo.

  • Hakikisha wasikilizaji wako wanaweza kuona vielelezo vyako. Kwa mfano, ikiwa utaonyesha picha jukwaani hakikisha ni kubwa vya kutosha ili wasikilizaji waweze kuiona.